Jazz


Jazz ni aina ya muziki iliyoanzishwa nchini Marekani. Jazz huunganisha tabia za muziki ya Kiafrika pamoja na tabia za muziki ya Ulaya.
Historia
Jazz ilianza mnamo mwanzo wa karne ya 20 Marekani. Kati ya vyanzo vyake ni muziki ya wamarekani weusi waliowahi kutunza muziki ya kiafrika kati yao kutokana na mababu waliopelekwa kama watumwa kutoka nchi za Afrika Magharibi. Pamoja na hayo walitumia pia sehemu za muziki ya Wamarekani wazungu yenye asili ya pande mbalimbali za Ulaya. Watalaamu kadhaa huitwa muziki yenye sauti ya Kiulaya pamoja na mpigo wa Kiafrika.
Neno la "jazz" kwa muziki ilitokea mara ya kwanza mjini New Orleans iliyoenea kutoka hapa katika maeneo jirani na miji mikubwa ya Marekani. Staili ya kusini ya Marekani iliitwa wakati ule "dixiland" kutokana na jina kwa ajili ya kusini ya nchi hii.
Kutoka asili hizi kuna aina nyingi za jazz zilizoendelea.
Wanamuziki mashuhuri
Wanamuziki muhimu wa Jazz ni pamoja na:
Wapiga tarumpeta:
- Louis Armstrong
- Bix Beiderbecke
- Miles Davis
- Dizzy Gillespie
Wapiga saxophone:
- Lester Young
- Frankie Trumbauer
- Dexter Gordon
- Stan Getz
- Ornette Coleman
- John Coltrane
- Charlie Parker
Wapiga trombone:
- Glenn Miller
- J.J. Johnson
- Curtis Fuller
Wapiga klarineti:
- Artie Shaw
- Benny Goodman
Wapiga piano:
- Count Basie
- Duke Ellington
- Thelonious Monk
- Chick Corea
- Oscar Peterson
- Eubie Blake
- Art Tatum
- James P. Johnson
- Fats Waller
Wapiga gitaa:
- Charlie Christian
- Joe Pass
- Django Reinhardt
- Wes Montgomery
Wapiga ngoma
- Jo Jones
- Art Blakey
Waimbaji
- Bessie Smith
- Ella Fitzgerald
- Duke Henderson
- Billie Holiday
- Sarah Vaughan